الأربعاء، 22 أبريل 2009

NADHARIA YA TAKWIMU YA LUGHA YA KUDURUSU MTINDO

NADHARIA YA TAKWIMU YA LUGHA YA KUDURUSU MTINDO


Hakika nadharia ya takwimu ya lugha ya kusoma mtindo unaweza kudurusu mitindo yoyote mtazamo unaotiliwa mkazo na mtafiti, kati ya mambo ambayo nadharia ya takwimu inajengwa juu yake ni kwamba matini ya fasihi kwa mtunzi maalum au katika elimu ya kifasihi maalum ina baadhi ya mambo muhimu yanayohusiana na lugha, kati yake ni:

1-Utumiaji wa mambo yanayofanana na maneno yaliyokuja ndani ya kamusi.
2-Kuongeza au kupunguza katika kutumia baadhi ya maneno maalum.
3-Urefu wa sentensi au ufupi wake.
4-Urefu wa maneno yanayotumiwa au ufupi wake.
5-Aina za sentensi (sentensi ya jina –sentensi ya kitenzi)
6-Athari ya mpandano wa maneno au vinyume na kuazima maneno maalum.

Kwa ufupi tunaweza kusema kwamba ufahamu wa mtindo kutokana na nadharia iliyotangulia inahusiana zaidi na maana ya kutohakikisha(intimali).
Masomo ya kimtindo yanatumia njia ya kukusanya nyanja kadhaa tunataja baadhi yake kama:

1-Usaidizi katika kuchagua aina kwa kuzichagua uchaguzi nyeti pale ambapo zinahusiana jamii inayotakiwa kusoma.

2-kupima kuzidi kwa sifa za kimtindo katika kazi mahususi, basi tunapotaka kupima kuzidi kwa sentensi ya jina katika matini mahsusi tunasimama kwa kupima idadi ya sentensi iliyokaririwa, kisha tunaigawanya juu ya urefu wa matini kutokana na idadi za sentensi ndani yake.

3-kupima kiasi kati ya idadi ya kutaja kwa sifa maalum ya kimtindo na idadi ya kutaja kwa sifa nyingine kwa ajili ya kulinganisha kati yao na njia hiyo inayofanywa kwa kugawanya kwa kukusanya idadi ya maana za kutaja kwa mojawapo zaidi ya sifa nyingine na kwa njia hiyo tunaweza kuhesabu nisba ya sifa nk.




Mtunzi anajaribu katika nadharia hii kutoa jambo jipya juu ya msingi wake inaweza kutenganisha (kupambanua) baina ya mitindo kwa mfano:

1-Kutenganisha baina ya lugha ya fasihi na lugha elimu.
2-Kutenganisha baina ya lugha ya ushairi na lugha nathari
3-Kutenganisha kwa lugha zinazotumiwa kupitia aina za kifasihi.

Na mwisho wa lengo lililokusudiwa, na mwana elimu wa Ujerumani Busemann ni kwamba inawezekana kupambanua kwa matini ya kifasihi kwa kuainisha kwa nisba baina ya kueleza kwa tukio (vitenzi) na kueleza kwa kutumia sifa kwa kukusanya idadi ya vitenzi katika matini na idadi ya sifa, na matokeo ya njia hii ni kujua kwa idadi ambapo huenda zikazidi au zikapungu kwa mujibu wa kuongeza au kupunguza idadi ya vitenzi juu ya idadi ya sifa. Nisba hiyo inatumia kwa kuzingatia kama ni dalili ya juu ya ufasiri wa mtindo, na kama nisba hiyo imeshaongezwa ilikuwa mtindo wa lugha ni karibu zaidi na mtindo wa kifasihi na inapopunguzwa itakuwa mtindo ni karibu zaidi na mtindo wa kielimu na njia ya Busemann kama yafuatayo:

Nisba ya kitenzi kwa sifa =idadi ya vitenzi ÷ Idadi ya sifa

Na njia hii inafupishwa ( N T S ) pale ambapo
N=kiwango T=kitenzi S= sifa, na ngeli ya vitenzi inakusanya vitenzi vyote isipokuwa vitenzi visaidizi. Na ngeli ya sifa inakusanya maneno yote yanayokuja kama ni fasihi katika kuzungumza ( sifa + yanayosifiwa ) na inakusanya pia maneno yanayotenda kazi ya sifa.

Na katika matokeo ambayo mtunzi amewasili kwake kwa methodolojia yake ya kilugha ni:

1-Unaweza kupambanua kwa jinsia ya mtunzi kama ni mwanaume au mwanamke.

2-Unaweza kujua umri wa mtunzi kama ni kijana au mzee (sheikh).

3-Unaweza kurejesha matini zisizo na mtunzi kwa mwanzo wake.

4-Kupambanua kati ya amali ya kifasihi na amali ya kisayansi.


(Aina za mitindo)

Maulamaa wamejitahidi katika kugawanya mitindo ya lugha na madhehebu yao yamekuwa mbalimbali katika kuigawanya kutokana na maono yao.

Baadhi yao wamegawanya mitindo kwa upande wa mtazamo wa kilugha kama mitindo ya sharti, ulizo n.k. Kutokana na mitindo ya kilugha.

Baadhi yao wamegawanya mitindo kwa upande wa mtazamo wa kilugha kama mitindo ya tashbihi, kina ya istiana n.k.

Na baadhi yao wamegawanya mitindo kwa upande wa kazi zao kama mitindo inayohusiana na maisha kwa mfano mitindo ya miamala ya watu , mitindo ya kielimu na ya kijamii.

Na baadhi yao pia wamegawanya mitindo kwa upande wa mitazamo ya kifasihi kutokana na malengo ya mwandishi, kwa mfano mitindo ya kisa, makala n.k.

(Mitindo ya kikazi)

(Nadharia ya mitindo ya kikazi kama ilivyokuja na, BARTH 1969).

Nadharia hii inafahamisha kwamba nidhamu yoyote ya kilugha ina malengo yanayofanana lakini malengo hayo yanagawanyika kutokana na mambo yanayoashiria mazungumzo kwa mfano, shughuli ya mawasiliano inaitwa mtindo wa mazungumzo n.k.
Na matokeo ya hayo yaliyotangulia tunakuta kwamba mitindo ya kilugha ambayo mtu anayatumia yanabadilishwa kama maudhui ikibadilishwa kwa upande mmoja na wanaoshiriki katika mazungumzo au wasikilizaji wake kwa upande mwingine, mitindo inageuzwa vile vile na vipengele vingine, baadhi ya vipengele hivyo ni vipengele vya jamii, kisaikolojia au vyote viwili, vilevile mitindo yanatofautina kutoka na aina ya kifasihi ambayo mwandishi anaizungumzia, pia mwandishi ana umuhimu mkubwa katika kutofautisha mitindo.
Masomo ya kilugha yamebainisha kwamba mitindo tofauti ni matokeo kwa hali ya kijamii mahususi, wanafalsafa wanaiita (sharti ya kijamii), yaani kila mtindo ni tokeo la kijamii una sifa za kijamii zenye malengo mengi na tofauti. RIEZEL amepambanua kati ya kazi tano za kimtindo kutokana na kazi zake za kijamii nazo ni:

1-Mtindo wa miamala wa kinasimu kwa mfano, balagha, hadithi za kinasimu na kanuni.
2-Mitindo ya kielimu kwa mfano, mihadhara ya kielimu na ya kisanaa.
3-Mtindo wa magazetini na uchapishaji, na kati yake maoni ya wanahabari na ukosoaji wa habari.
4-Mtindo wa miamala ya kila siku na humathilisha (kufananisha) katika mazungumzo ya watu na mawasiliano yao wenyewe kwa wenyewe.
5-Mtindo wa sanaa nzuri unamathilisha katika matini za kifasihi.

MARTIN JOOS ameongeza aina mbili za mitindo ya kikazi katika aina zilizotangulia nazo ni:

1-Mtindo wa ushauri utumiao kati ya hakimu na washauri wake au mawaziri wake wakati wa kujadili kuhusu mambo ya dola.
2- Mtindo wa upendo na malengo yake ni kuzungumza zaidi juu ya yaliyo ndani ya moyo kama mapenzi, na mtindo huo ni mtindo utumiao kati ya mume na mke (wanandoa) na wanaoishi katika familia moja.

Na katika nyanja ya lugha ya Kiswahili MAW.J mwaka 1974 amegawanya mtindo wa nathali ya Kiswahili katika:

1-Mtindo wa maneno yaliyosemwa. Na mtindo huo una baadhi ya sifa kama kuzitumia sentensi zenye urefu au ufupi, kukithiri kwa kutumia viambishi vya kurejea na kutumia vivumishi vya kuonyesha kabla ya jina.
2-Mtindo wa maneno yaliyoandikwa na mtindo huo una idadi kadhaa za vipengele vya kilugha katika ibara ya sentensi wastani.

MAW.J amegawanya mitindo ya nathari kwa ujmla katika mitindo mine:

1-Mtindo wa kwanza:
Mtindo wa munadhama na mtindo huo una baadhi ya sifa kama kuzidisha idadi za vipengele vya kitenzi juu ya vipengele vya kijina.

2-Mtindo wa pili:
Mtindo wa kukamilisha na mtindo huo una baadhi ya sifa kama setensi zenye ibara mmoja na kuwepo kwa vipengele vya kijina kwa uwazi.

3-Mtindo wa tatu:
Mtindo wa visa na mtindo huo una baadhi ya sifa hasa kama kuwepo ibara tofauti pamoja na ongezeko la nisba ya ibara ya kitenzi na kutumia kwa vivumishi vya kuonesha na vivumishi vya kumiliki kabla ya jina.

4- Mtindo wa nne:
Mtindo wa mazungumzo unaotambuliwa kwa ibara zake zilizofungamana na sentensi zake fupi na tamko lenye neno moja.

Kwa hivyo tunaona kwamba MAW.J amegawanya mitindo kwa upande wa kazi zake kutokana na maudhui ambayo mwandishi au msemaji anazungumzia juu yake, na kwa kuangalia tunaona kwamba yeye ameegemea katika uchunguzi wake juu ya kutafsiri kwa kilugha na upande wa kifasihi haukuwa na nasibu (sehemu) yoyote katika uchunguzi huo.

Na kwa upande mwingine MWANSOKA 1991 ameigawa mitindo katika lugha ya Kiswahili, katika vigawanyo vinne vya kazi navyo ni:

1-Mtindo wa kitaaluma:
Unahusisha na mtindo wa vitabu vya shule, majarida mahususi,mtindo wa mihadha ya chuo kikuu, vikao vya uchunguzi, ripoti na ujumbe wa kielimu .

2-Mtindo wa kirasmi:
Unahusisha na mtindo wa mazungumzo kazini, mikutano ya kidiplomasia, kanuni, mikutano na uamuzi wa kiserikali

3-Mtindo wa magazeti na shughuli za kisiasa.
Unahusisha na mtindo wa majarida ya kitaifa na ya kichama, majadiliano ya bunge na mikutano ya chama.

4-Mtindo wa mawasiliano ya kawaida (yasiyo rasmi).
Uhusiano na mtindo wa maisha ya kila siku baina ya watu na nyumbani na baina ya wasafiri na marafiki.

Kutokana na migawanyo hiyo ya kikazi tuliyotanguliza kwa mitindo tunatoka kwa mgawanyo wa kikazi kwa mitindo inayojegwa juu ya yaliyotangulia nayo ni:
1-Mtindo wa kirasmi. 2-Mtindo wa magazeti.
3-Mtindo wa kishauri. 4-Mtindo wa kitaaluma.
5-Mtindo wa miamala wa kirasmi 6-Mtindo wa fasihi nzuri.
kutokana na migawanyo ya mitindo kwa upande wa kazi, tunaleta miganyo ya mitindo kwa upande wa fasihi, nayo ni.

(Mitindo ya kifasihi)

Mtindo wa mtazamo wa lugha ya fasihi juu ya lugha inayoandikwa au fasihi tu, bali unafungamana na sharti la jamii kwa mujibu wa hitilafu ya tabaka za kijamii na utamaduni zinazohitilifiana.

Ni wajibu kuuliza juu ya mtindo wenye methali ya kifasihi, je faida na sifa za kueleza zinakuja katika methali ya kifasihi zinakwenda sambamba pamoja na mitindo au la?
Hakika lugha ya kifasihi inakwenda kinyume na lugha ya mawasiliano ya kila siku nayo ni yenye kufahamika zaidi na yenye kukusudiwa katika kujengwa kwake, kwani fasihi inatumia lugha utumiaji mzuri sio wa mawasiliano.
Na hiyo inatuelekeza kwa kuonesha migawanyo ya mitindo kwa upande wa kifasihi kwani kutofautiana kwa mitindo ya kifasihi kunarejea kwa sababu mbili:

Ya kwanza: maudhi
Nayo ni fani ya kifasihi ambayo mwandishi anachagua kwa ajili ya kueleza kwa yaliyo ndani yake na kwa upande wa elimu,fasihi, shairi na nathari, basi kila moja kati yake ina mtindo wake mahususi ambao hujulikana kwake na kwenda sambamba pamoja na tabia yake ya kifasihi.


Ya pili: mwenye fasihi.
Hitilafu ya mtindo hapa inarejea kwa hitilafu ya akili za wenye fasihi, tabia zao na njia ya fikra zao na Dokta,Ash shayb (1939) amegawanya mitindo kwa upande wa kifasihi katika mtindo wa kielimu na mtindo wa kifasihi, na amegawanya mitindo ya nathari katika migawanyo miwili.

Ya kwanza: Nathari ya kielimu.
Nathari hiyo ina sifa zake zinazoitambulisha na inachukuliwa kama njia ya kueneza maarifa, na maarifa ya kiakili ni msingi wake na mara chache unakuta athari ya ghadhabu ndani yake.



Ya pili: Nathari ya kifasihi.
Nathari hiyo inatambuliwa kwa kuingiza hisia ndani yake pamoja na kuingiza hakika na fikra zenye umuhimu zaidi nayo ni lugha ya hisia na lengo lake ni kuchochea kwa hamasa katika nafsi za wasomaji na wasikilizaji.

(Mtindo wa maisha ya kibinafsi)

Ama mtindo wa maisha ya kibinafsi ambao uchunguzi unakuwa juu yake, basi Dk Ash shayb ameijaalia katikati baina ya mtindo wa kitaaluma na mtindo wa kifasihi, basi ikiwa mtindo wa maisha ya kibinafsi unakutwa ndani yake mtindo wa kitaaluma na kifasihi,basi kwa nini usiwekwe mgawanyo mwingine wa mtindo ambao unakusanya kati ya mitindo miwili ya kitaaluma na kifasihi? Nasi tuna mtindo unaoumathilisha nao ni mtindo wa maisha ya kibinafsi.

Na maisha ya kibinafsi ambayo Dk Abdul-Aziz Shah ameiita kwa jina la maisha ya kibinadamu amezigawanya baadhi katika migawanyo miwili.

Maisha ya wengine:
Nayo ni utafiti juu ya hakika katika maisha ya mwanadamu hodari na kuchambua kwa uhodari wake,siri zake au siri za uhodari wake toka katika hali ya maisha yake na matukio aliyoyakubali na athari aliyoiacha katika rika lake.

Maisha ya kibinafsi:
Mwandishi mwenyewe anaandika maisha yake ya kibinafsi hali ya kufichua pia siri za maisha yake ya ndani na kutazama kwa makini kwa nafsi yake inayojumlisha kwa kuwepo utajiri wa ndani, na sifa zinazojaalia maisha ya kibinafsi ni kubwa sio sifa zinazojaalia maisha ya wengine kuwa ni kubwa. Na sifa kuu kati ya sifa hizo ni kuwa mwandishi wa maisha ya wengine, ana mtazamo wa maudhui anatambua kwa haraka,anafahamu kwa makini na anajua uhakika wote na anatoa hukumu juu yake.
Ama mwandishi wa maisha ya kibinafsi naye ana ubinafsi kabla ya kila kitu naye anatazama nafsi yake kwa uangalifu.
Dk Ash Shayb anasema kwamba maisha ya kibinafsi yanahesabu historia inayohusiana na maisha ya watu na mpango wake unafuata njia tatu.


Ya kwanza: Mwenye historia anaandika katika maisha ya mwingine, basi anachagua matukio na athari na anazipanga na anazifasiri.

Ya pili: Mwenye historia anachagua njia isiyo ya moja kwa moja naye anaficha nyuma ya maudhui ili ajaalie aoneshe nafsi yake,basi anatuonesha maneno ya mtu, maoni yake, madhehebu yake ya tabia,marafiki zake, wanafunzi wake, mashairi yake na athari yake bila ya kuzungumza kwa kuzikosoa na kuzichambua.

Ya tatu: Mwenye historia anaandika maisha yake mwenyewe kwa kalamu yake, basi anzungumzia juu ya hakika na anafasiri matukio aliyoyapita kwa upande wa mtazamo wake mwenyewe.

Na yaliyotangulia yanaonesha kwetu kwamba mtindo unagawanywa ima kwa njia ya kazi yake ya kijamii au kwa njia ya fani ya kifasihi ambayo mwenye fasihi anazungumzia na inachukuliwa wakati wa kusifu mitindo hiyo, chanzo chenyewe au mwenye fasihi au yaliyozunguka kwake kati ya hali ya kijamii na uwezo wa mwandishi unasimama muelekeo wake wa kifasihi, utamaduni wake, enzi yake na uhusiano wake wa kijamii.

Mtindo wa maisha ya kibinafsi juu ya viwango vitatu:

1-Kiwango cha neno
2-Kiwango cha mitindo ya kilugha
3-Kiwango cha picha za kibalagha.

Na kutokana na hayo yaliyotangulia tunakuta kwamba kila mwenye fasihi ana mtindo wake maalum.

Imetimiza


Wanafunzi waliofanya kazi hiyo ni:

• Abdallah Elashry
• Ali Gabr
• Ramadam Mosa
• Ramy Adbel Salam
• Mohammed Abbas

هناك تعليقان (2):

  1. برافو جدا.. ربنا معاك ويوفقكم.. كل في تخصصه هنخدم المتخصصين في الشأن الأفريقي والمهتمين بالتخصصات الأفريقية المختلفة.. تحياتي أخوكم الصعيدي حماد فوزي-جامعة القاهرة والأصل جامعة الأزهر

    ردحذف
  2. جزيل الشكر دكتور حماد واعتذر لتاخرى فى الرد على سيادتكم

    ردحذف

My Own Room


Go Large!
بروف عباس يرحب بكم على المدونه الالكترونيه الخاصه به profabbas.blogspot.com ويرحب باستفساراتكم على الايميل الخاص به professor_abbas@hotmail.com