الأربعاء، 22 أبريل 2009

Maana ya mtindo na nadharia zake

MAANA YA MTINDO NA NADHARIA ZAKE

Maoni mbali mbali yamekuja katika maana ya mtindo,na wanavyoni wamegawanyika kwenye madhehebu mengi.

Maana ya kwanza:
Mtindo ni njia ya utekelezaji wa maana.

madhehebu hiyo imeunganisha kati ya mtindo na njia za utekelezaji wa maana pale ambapo kila msimamo maalum asemao.
Na uhitilafu wa mitindo hapa unarejea kwenye hitilafu ya msimamo na tabia ya maudhui na uwezo wa mwandishi wa kisanii.
Miongoni mwa wafuasi wa madhehebu hiyo ni Ibn Qutaibah, pale ambapo ameunganisha kati ya mtindo na lengo ambalo mwandishi anajizungumzia ndani yake, pia ameunganisha kati yake na hali ya mpokeaji na utamaduni wake.
Miongoni mwao ni Al-Baklani pale ameafikiana na Ibn Qutaibah katika kuunganisha mtindo kwa aina ya Fasihi katika njia za utekelezaji kila aina ndani yake, kutoka barua, ujumbe, shairi, nathiri na nyinginezo.
Na miongoni mwao Al-shaib, nao anaafikiana na walio mtangulia katika kuunganisha mtindo kwa sanaa ya Fasihi (Lengo la fasihi), kutokana na hayo ameigawanya mitindo kwenye mitindo yenye makala, hutuba, sira, kisa na nyinginezo.

Nadharia ya hitilafu ya kiwango cha lugha.

Nadharia hiyo inategemea juu ya hitimali kwamba usemaji wa lugha unahitalifiana kwa mujibu wa anaye zungumziwa na kwa mujibu wa aina ya uzungumzaji na maudhui yake.
Mfano wa hilo, mazungumzo ya kitaalamu au ya kisanii inahitilifiana na mazungumzo ya mpira wa miguu.
Nadharia hiyo ina uwezo muhimu katika tafsiri ya matini, nayo inaamiliana na maneno ya kilugha yaliyomo ndani ya kamusi ambayo ni maneno makhususi kwa mujibu wa hitilafu ya kiwango cha kilugha.
Lakini nadharia hiyo katika wakati ule ule inasisitiza juu ya kitamko zaidi ya lugha ya kimaandishi, na hakuangalia kwenye miundo ya kinahau kwa umbo la kijumla.



Maana ya pili:
Mtindo ni kuchagua kwa miundo ya kilugha na kuunga baina yao katika matini.

Kuchagua katika mtindo ni kuchagua kwa mwandishi kwa neno fulani pasipo na lingine kwani neno hilo ni karibu zaidi kwa maana au mwandishi anapendekeza neno au maumbo ya kinahau kwani umbo hilo ni sahihi zaidi kinahau na kimaana.
Ama kuunga ni kujaribu kuunga baina ya maneno ndani ya sentesi kwa ajili ya kufikia maana inayotakiwa kwa makini na uwazi.
Na kwa maana hiyo tunakuta kwamba mtindo -katika madhehebu hiyo-inachunguzwa kupitia kwa matini ya maandishi tu pasipo na kushughulika kwa mwandishi au anayepokea.
Miongoni mwa wafuasi wa madhehebu hiyo ni Abdul-khahir Aljirjaniy.
Maneno yake ya mwisho kwamba mwandishi anachagua maneno ndani ya nafsi yake na anayewafikiana na maana anazipanga maana ndani ya nafsi yake na anaziweka kwenye umbo sahihi la kinahau na anajenga baadhi yake juu ya baadhi nyingine kwa ajili ya kuonyesha juu ya fikra anayeitaka. Abdel kaher amejaaliwa kuchagua kwenye lafudhi (maneno) na kuunga baina ya maneno kwa ajili ya kupata fikra sahihi anayotaka kueleza na anajalia mtindo anakusanya lafudhi na maana, kuchagua kunakuwa kwenye lafudhi na kuunga katika maana.
Na miongoni mwao Ibn Khaldon amesisitiza juu ya lafudhi kwani ni zinabainisha maana inayotakiwa kwani maana inapatikana katika lafudhi, na uwezo wa mwandishi katika kuzichagua lafudhi kwa njia sahihi na kuunga baina yao ni ambazo zinavuta kwa maana ya kina zinazokusudiwa na hapa tunamkuta ameafikiana na Abdel Kahr katika kuchagua na kuunga baina ya lafudhi pamoja na kulazimika na mahusiano ya kinahau baina yake.

Maana ya tatu:
Mtindo ni mtu.
Maana hiyo inategemea juu ya maisha ya mtungaji, sera zake mwenyewe, na umeizingatia ni msingi muhimu katika uchunguzi na utafiti. Na kunashughulikiwa pia na jamii ya mwandishi utamaduni wake na majaribio yake.
Miongoni mwa wafuasi wa madhehebu hayo ni Ibn Al-athir kwani mtindo wenyewe unategemea uwezo wa mwandishi katika kueleza yaliyo ndani yake kwa njia nyingi Ibn Al-athir ameunganisha kati ya mtindo na kati ya mwandishi na uwezo wake wa kisanii, na kuutumia uwezo huo katika kuonesha fikra katika mitindo mizuri na njia mbalimbali, pale ambapo tunaweza kuiona hitilafu hii katika kuonesha fikra moja kwa waandishi wawili waliohitilifiana, kila mmoja kati yao anaitumia kwa mtindo wake maalum, au mwandishi anatoa fikra hiyo hiyo kwa njia mbali mbali.
Na miongoni mwao ni Boffun yeye amesema kwamba mtindo ni mtu. Maana hiyo inaungaisha baina ya mtindo asili yake kwa upande wa vipengele vya kisaikolojia, kiutamaduni, na kijamii. Naye anakusudia tabia ya mtungaji, uhakika wake, na ufahamu wake wa kilugha.
Naye anaelezea mtindo hapa. Kama ni njia ya mtungaji mwenyewe au mwenendo wake katika maandiko. Na juu ya maana hiyo imeundwa nadharia ya mtindo wa mtu: Nadharia hiyo imesimama juu ya msemo kwamba mtindo ni mtu. Na kwa maana hiyo tunaweza kuainisha kutokana na mtindo saikolojia ya mwandishi, upendeleo wake, matakwa yake, na muundo wa kisaikolojia, unaozifanya zana zake za kiisimu zinachukua njia hiyo au ile.
Nadharia hiyo inamtakia mtafiti wa mtindo ujuzi wa ukamilifu kwa maisha ya mtungaji, sera yake mwenyewe, jamii yake na enzi yake ya kihistoria.
Na hayo kwa kawaida inamchukua mtafiti nyanja nje ya ile anayoitafiti ndani yake. Na hayo sio rahisi kuitekeleza kwa namna njema katika muda unaokubalika. Kwa upande mwingine, mchunguzi katika nyanja ya mtindo hawezi kukaribu na matini ambayo mtungaji wake hakujulikana ili kuisomesha. Kutokana na hayo ni vigumu kuitekeleza nadharia hiyo juu ya matini ya fasihi kwa jumla.

Maana ya nne:
Mtindo ni kiongezi kizuri na ni ziada ya kuelezea.
Na ziada ya kuelezea inabainika wakati wa unganishi kati ya misemo miwili, ya kwanza ni msemo usiokuwa na kielezea na inatekeleza maana tu,
ya pili inatekelezea maana hiyo hiyo, lakini mwenyewe ameitengenezea na ameipa mifano.
Na kwa msingi huo, mtindo hapa ni kiongezi cha kielezea chenye kuathiria vipengele vya lugha kisiokuwepo hapo kabla na kinachozidi kutokana na nguvu ya maana na athari yake. Miongoni mwa wafuasi wa madhehebu hii Charle Bally, naye ameona kwamba mtindo ni kiongezi kizuri na ziada ya kielezea, na mtindo wenyewe unadhihirisha katika kundi la vipengele vya lugha vyenye uathiri wa kipenzi juu ya msikilizaji au mwandishi.






Shule ya mtindo wa kielezea

Shule hiyo inalingana na, ambayo kiongozi wake ni Sharle Bally, utafiti wa vipengele vya kielezea vilivyofichika au vilivyochochekea ndani ya maneno. Kwa mfano. Kauli yako, nenda hilo, naapa kwa mola wako nenda hilo, ni starehe na nenda hilo. Pamoja na maneno hayo yote yametekelezea kwa kitendo cha amri kilichopelekwa kwa anayesemwa wa kiume, isipokuwa vidokezo, vihushio, vinaashiria, vinadhihirisha mambo mbalimbali vya upenzi. Shule hiyo imejitenga na kutafiti katika matini ya nathiri ya kisayansi ambapo kawaida haisifika na kuwepo mapenzi ndani yake. Na utekelezo wake umeshughulikia na vitamkwa zaidi kuliko maandishi, na wala haishughulishwa na maandishi mapya ya kifasihi. Kwa hivyo haiwezekani kwa shule hiyo kutekeleza maendeleo makubwa katika utafiti wa kimtindo au utafiti ukamilifu juu ya mtindo.

هناك تعليق واحد:

  1. أنا كمان هعملكم نشر للمدونة دي المتخصصة في الشأن الأفريقي باللغة السواحيلية.. أي خدمة أنا موجود يارجالة.. ربنا يجعلنا في خدمة الآخرين المهتمين بالتخصصات الأفريقية

    ردحذف

My Own Room


Go Large!
بروف عباس يرحب بكم على المدونه الالكترونيه الخاصه به profabbas.blogspot.com ويرحب باستفساراتكم على الايميل الخاص به professor_abbas@hotmail.com